HADITHI NZURI YA KUSISIMUA: SIKUMBUKI




Siku moja nikiwa nimekaa na marafiki zangu tukiwa tunabadilishana mawazo mara ghafla nilimuona mdogo wang akikimbia kwa kasi sana kuja pale tulipokuwa na marafiki zangu na alipofika ghafla akasema

Mdogo wanu: Kaka mama

Mimi: Kuna nini mdogo wangu?

Mdogo: mama yupo kule

Mimi: wapi hebu sema haraka maana sikuelewi?

 Kwa hakika mdogo wangu alishindwa kusema ni nini kilichotokea hivyo tukatoka pale moja kwa moja na marafiki zangu tukiwa tunamfuata mdogo wangu Ally ambaye alikuwa katangulia mbele yetu huku akilia, sikuweza kuelewa kwa maana sikuwaza kama kingetokea kilichotokea siku ile.

 Tulitembea kwa muda wa dakika tano kisha tukafika nyumbani nilipokuwa nikiishi na mama yangu na mdogo wangu.

 Laaaah! Sikuamini nilichokiona mbele yangu kwa maana mama alikuwa amelala yuko hoi hajitambui, ghafla nilishikwa na bumbuazi kwani nilipojaribu kuangalia mapigo ya moyo wa mama tayari yalikuwa yameshasimama .

 Nilikosa nguvu na kujikuta naanza kulia kama mtoto lakini kwa wakati huo mdogo wangu alikuwa analia sana na sikupata ujasiri wa kumueleza kuwa mama ambaye kwake alikuwa ni dada yake kipenzi Tayari ameshaaga dunia nilichokifanya nilitoka nje bila kumsemesha mtu yeyote na kwenda kwa Mjomba ambaye alikuwa karibu na pale nyumbani kwetu. Nilipofika nikamkuta yupo anacheza na mtoto wake wakiwa na furaha kubwa, basi nikaona siyo vyema nikamueleza kuwa mama ameshaaga dunia. Nilitoka pale nyumbani kwa mjomba hali ya kuwa sijitambui.

Nikiwa njiani mara ghafla niliona ni kama ndoto kwa maana nilipozinduka nilijikuta nipo hospitali mguu ukiwa umevunjika na pia nilikuwa nimewekewa pamba maskioni ishara ya kuwa tayari nilikuwa mfuu.

Hivyo kutokana na kwamba nilihisi mambo yote yalikuwa ni kama ndoto nikatoka pale sehemu ambayo ilikuwa ni monchuary, basi nilitoka pale lakini baada ya kufika pale mlangoni nilianza kugonga mlango kwa maana ulikuwa umefungwa kwa nje, niligonga mlango zaidi ya maya kumi lakini hapakuwa na mafanikio yoyote.

Baada ya kuona kuwa hakuna wa kunifungulia nilibadili nguo na kuvaa nguo ambazo zilikuwa pale ndani kisha nikaelekea kwenye dirisha lilikuwa pale ndani kisha nikalifungua nilipochungulia nikamuona nesi mmoja alikuwa anasafisha madirisha ya pale kwenye mjengo.

Upande wa pili marafiki zangu waliwataarifu majirani na watu wengine kuwa mama yangu ameshafariki dunia  hivyo walianza kufanya maandalizi ya kumfanyia mazishi mama.

Haikuwia vigumu kufanya maamuzi juu ya kumzika mama yangu  kwani katika familia yetu tulikuwa wawili tu, mimi na mdogo wangu Ally

Wakati huo mimi nilikuwa naelekea nyumbani sasa kujua ni kipi kinachoendelea huku kichwani nikiwa na makovu kichwani.

Nilifika nyumbani na kuwakuta watu wamekaa huku wakilia kwani mama yangu alikuwa akiishi na majirani zake vizuri hakuwahi kugombana na mtu yeyote katika kijiji chetu cha MANDONDE kutokana na sifa hiyo ya mama basi ilitufanya kupendwa sana na majirani zetu hasaaa mdogo wangu Ally ambapo yeye alikwa ni mtoto mtiifu sana pale mtaani kwetu.

Dah baada ya kufika pale nyumbani watu walishtushwa sana na ujio wangu, kwani mwili wangu ulikuwa umejaa makovu baada ya kufika tu ghafla ukimya ulitawala na wale waliokuwa wakilia wote walinyamaza ndipo hapo akanyanyuka mama mmoja ambaye alikuwa ni rafiki mkubwa sana na mama yangu na kisha akanifuata nilipo na kuniuliza

Mama: Mwanangu kimekusibu nini mpaka umekuwa kwenye hali hii.

Dah swali la mama Yule lilinifanya kudondosha chozi kwa maana nilimkumbuka mama yangu ambaye kwa muda huo alikuwa anaandaliwa na safari yake ya mwisho, nilianza kutiririkwa na machozi kiasi ammbacho nilisababisha hata Yule mama nae aanze kulia.

 Alikuja rafiki yangu Harry na kuniuliza kuwa ni nini kimenitokea?

 Nikamwambia wakati nilipotoka pale ndani nilikuwa nikielekea kwa mjomba HASHIMU kumueleza juu ya kifo cha mama lakini baada ya kufika kwa mjomba nilimkuta yuko anacheza na mwanae hivyo nikaona siyo ningefanya vibaya kumpa taarifa ile ambayo ingeharibu furaha yake, sasa mda ule natoka kwa mjomba  baada ya kutembea hatua kadhaa kutoka getini kwa mjomba sikujua ni nini kilichonitokea bali nilijikuta tu nipo sehemu ya kulaza maiti.

 Harry: Enheee baada ya hapo nini kikatokea?

 Mimi: unh baada ya hapo nikanyanyuka na kutoa pamba zilizokuwa maskioni na puani kisha nikavaa kuna hizi nguo ambazo zilikuwa pale ndani lakini wakati nataka kutoka………………

 Mjomba: Ahmed umekuwaje mjomba

Mimi: nimepata ajali kidogo wakati nakuja kukupa taarifa Juu ya kifo cha mama nikiwa njiani nikagongwa na gari kisha watu wakanipeleka hospitali, niliogopa kumueleza mjomba kuwa mimi tayari nilikuwa ni mfu aliyefufuka nikaamua kuishia hapo.

Baada ya kumwambia vile mjomba alinishika mkono na kwenda nae mpaka ndani ulipolazwa mwili wa marehemu mama yangu.

Kisha ukawa ni muda wa kuuga mwili wa mama yangu na baada ya hapo ikawa ndiyo mwisho wa kumuona mama yangu.

Watu walitoka nje huku wakiwa wamebeba jeneza ambayo ilikuwa ni usafiri wa kumsafirisha mama yangu na safari yake ya mwisho, pembeni yangu alikuwa mdogo wangu Ally ambaye yeye wala alikuwa haelewi ni nini kinachoendelea.

Baada ya kumzika mama yangu tulirudi nyumbani huku nikiwa na majonzi moyoni na pia huzuni usoni.

Siku hiyo mpaka usiku watu walikuwa bado wapo pale nyumbani wakijadili juu ya msiba wa  mama.

 Siku ya kwanza ilipita watu wakazidi kupungua siku ya pili nayo watu wakapungua tena tukabaki ndugu na majirani wa pale karibu na nyumbani na siku ya tatu ilipofika watu walikuja wengi wengi na kisha  tukaomba dua kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 4 asubuhi baada ya hapo watu walipata sadaka ya pilau Kwa nyama, wale wa kula kwa kukomoa nao walikula lakini pia wale wa kubeba chakula kupeleka majumbani mwao walifanya hivyo.

Siku ya siku ilipofika nilijikuta nimebaki mimi na mdogo wangu Ally tu pale nyumbani.

Mchana wa siku hiyo nilikuwa nimekaa kwenye mti karibu na nyumba yetu nilimuona mdogo wangu Ally akiingia ndani kisha baada ya kuingia ndani akaanza kumuita marehemu mama.

 

Dah! Hakika iliniuma sana haraka haraka nikashuka mtini na kuelekea alipo Ally  kisha nikamuuliza unalia nini? Akasema kuwa njaa inamuuma nikamwambia usijali twende huku.

Tulitoka pale na kuelekea kibanda walichokuwa wanapika chakula kisha nilimuomba mhudumu ampe Ally chakula ambacho kingemtosheleza akapewa chakula akala akashiba lna hapo wazo tena la kumtaka mama hakuwa nalo tena..                                                                                                                                                                                                                                                                                                              

 Tulitoka pale wanapouza chakula kisha tukarudi nyumbani  tulipofika tu Ally aliingia ndani kisha akawa amelala.

Nikiwa nimekaa pale mlangoni mara ghafla kichwa kilianza kuuma kiasi kwamba nilihisi kichwa kinataka kupasuka na baada ya dakika kadhaa nikaanza kuona Mawenge kiasi kwamba hata kitu kingepita mbele yangu nisingekiona.

 

Baada ya muda nilirudi katika hali yangu ya kawaida lakini dah kila niliyemuona pale mbele yangu alikuwa ni mtu mgeni hakuna hata ambaye nilikuwa nikimjua.

Ndipo baada ya kuamka swali la kwanza niliwauliza nipo wapi? Na je nyie ni wakina nani?

Dah swali lile kwa hakika liliwaumiza sana wale waliokuwa pale kabla hawajasema chochote mara akaingia daktari aliyekuwa ameshika karatasi na baada ya kufika pale akasema kuwa nimepatwa na tatizo la kusahau kutokana na kwamba kuna uvimbe kwenye kichwa changu ambao ulisababishwa na ajali ya siku ile..

Nilikaa pale hospitali kwa muda wa siku tatu huku nikiwa sikumbuki kitu chochote lakini pale alipokuwa anakuja Ally nilikuwa nikimpenda sana japo nilikuwa simkumbuki lakini nilitokea kumpenda sana bila kujua alikuwa ni mdogo wangu.

Niliporudi nyumbani baada ya kupita siku kadhaa nikiwa hospitali basi kuna jirani yetu ambaye alikuwa ni rafiki mkubwa sana na mama yetu ambaye kwa hakika alimpenda sana Ally alimchukua na kuwa anakaa nae na niliporudi japo nilikuwa sikumbuki chochote ila aliniomba kuwa akae na Ally name kwa kuwa sikuwa nikimkumbuka nilikubali. Basi maisha yakaendelea.

 

MIEZI SITA (6) BAADAE

Siku moja nilikuwa nimekaa kwenye mti ule uliokuwa karibu na pale nyumbani basi ghafla mawazo nilijihisi wa tofauti maana kila kitu nilianza kukikumbuka baada ya ya Ally kuja na Kuniita kwenda kula chakula.

 

Nilienda  kula chakula kwa rafiki yake mama ambaye kwa mda huo nio alikuwa kama mama yetu.

Baada ya kumaliza kula nilimwambia “hakika mama nashukuru kwa wema wako ila naomba niseme kitu kimoja hakika wewe hauna tofauti na mama yetu hivyo nakuomba sana nisaidie kumtunza mdogo wangu kwa maana wewe sasa  ndiye mama wa mtoto huyu hana pengine pa kutegemea ijapokuwa kaka yake nipo lakini sina kitu na itaniwia vigumu kumtunza mdogo wangu tafadhali mama”

Mama: “usijali mwanangu huyu sasa ni kama mwanangu kama unavyojua kuwa mama yako sijabahatika kuwa na mtoto hivyo Ally nitamtunza, kumpenda, na kumjali kama mtoto wangu wa kumzaa”.

Dah! kwa hakika maneno ya mama huyo yalinipa furaha na kunifariji kiasi Fulani na kuamini kwamba mdogo wangu ataishi kwa furaha kubwa  maana hata baada ya kufa mama nilikuwa na wasiwasi ni jinsi gani naweza kumlea mdogo wangu hali ya kuwa sina kitu?

kisha nikamwambia “ nashukuru sana mama kwa Maneno yako mazuri na yenye faraja lakini pia nami nitakuwa najitahidi kadri niwezavyo ili kumlea mdogo wangu.

Nilitoka pale hali ya kuwa tayari nina amani tele moyoni.

Basi baada ya kutoka pale nilienda nyumbani na kisha nikaanza kutafuta vyeti vyangu vya shule pamoja na chuo ili kuhakikisha kama naweza kuvikuta kwa maana alikuwa navyo marehemu mama.

Lakini kwa bahati nzuri havikuwa mbali sana nilivikuta na kisha nikaviweka kwenye begi langu na kingine cha Ally ambacho kilikuwa ni cha kuzaliwa basi sikuwa na budi nilienda kumkabidhi Mama anae mlea mdogo wangu.

Usiku uliingia na mimi nilikuwa nikijiandaa na safari ya kuelekea mjini kwenda kutafuta kazi.

Basi nilipanda kitandani huku nikiwa natafakari nitaenda lakini sikujali kwa maana mfukoni nilikuwa na Shilingi laki mbili (200,000/=) hivyo nikaamini zingenisaidia huko nitakapoenda.

Kesho yake asubuhi na mapema  nilielekea kituo cha mabasi ambacho kilikuwa mbali kidogo na nyumbani hivyo ilinibidi kuamka mapema sana.

 

BAADA YA MIEZI MITATU

Nilikuwa katika ya jiji la Mwanza nikiwa sielewi ni njia gani nitafanya ilikupata kazi kwa maana nimejaribu kupita kila njia kwa hakika sikuona mafanikio, na nikikumbuka ni kiasi gani rafiki yangu ambaye tulisoma wote chuo alivyonisaidia na kunipa  hifadhi hivyo nikawa na wivu wa maendeleo juu yake nami nikatamani mda huo niwe kama yeye au nimzidi yeye hivyo kila siku nilikuwa ni wa kupita kwenye maofisi ya watu kutafuta kazi.

 

Siku zilipita miezi nayo haikubaki nyuma wakati huo nimekuwa nikimtegemea rafiki yangu Calvin ambaye ndiyo alikuwa msaada mkubwa kwangu.

 

Siku nikiwa niko nyumbani nimekaa mara ghafla simu yangu iliita na baada ya kuangalia ni Calvin alikuwa akipiga simu nikapokea:

Kisha sauti ikasikika “ samahani wewe ni ndugu wa mmiliki wa hii simu?

Nikamwambaia ndiyo huyo ni ndugu yangu kwani kimemkuta nini akasema ndugu yako alidondosha simu yake halafu mimi ndiye niloiokota

Dah! Kidogo nilipumu na ndipo nikapata nafasi ya kumuuliza kuwa ni wapi atakuwa yeye ili nikaichukue alinieleza na baada ya kunieleza nikaenda kuichukua simu yake kisha nikawa narudi nyumba.

Wakati nikiwa narudi nyumbani mara ghafla nilichomwa na kimti kilichokuwa ardhini ambacho kilisababisha mguu uane kutoka damu na hivyo nikajikaza kuelekea  nyumbani nikiwa niko barabarani mara ghafla kuna gari lilipita karibu yangu na kisha ikasimama mbele kidogo na baada ya kusimama dereva alishusha kioo na kuntoa mkono nje ishara ya uniita. Sikujua ni nani aliyekuwa akiniita lakini nilitembea haraka kuelekea gari lilipo nilipofika nilimkuta mama mmoja ambaye ni jirani yetu karibu na pale ninapoishi na Calvin kisha Yule mama akaniuliza

Mama: “mguu umefanyaje mbona unachechemea?”

Nikamwambia  kuna kimti kidogo kimenichoma tu ndio maana unaona nachechemea

Mama: ah basi panda nikupeleke mpaka nyumbani maana hata mimi naelekea huko huko

Nilishangaa na kumuuliza kwani mama unanijua mimi?

Akacheka kidogo kisha akasema wewe si unaishi na Calvin? Nikamwambia ndio basi story zikaendelea huku maswali ya hapa na pale yakiendelea mwishoni akaniuliza samahani kijana unaitwa nani?  Nikamwambia kuwa mimi naitwa Ahmedy naye akajitambulisha kama mama BINAJATI nikamwambia okay nafurahi kukufahamu lakini mimi naomba niishie hapa maana hapa kuna sehemu nataka nipite

Mama akasema hapana bwana twende kuna dawa pale nyumbani ukachukue angalau inaweza kukusaidia……

 

ITAENDELEA ………………………………..

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

  

Chapisha Maoni

0 Maoni